24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

DC AWATAKA MADAKTARI, WAUGUZI KUWAJIBIKA

Na SAMWEL MWANGA


MKUU wa Wilaya ya Maswa, Dk. Seif Shekalaghe amewataka

madaktari na wauguzi katika hospitali ya wilaya hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia maadili ya kazi zao.

 

Alitoa kauli hiyo kwa waandishi wa habari  baada ya kutembelea hospitali ya wilaya hiyo na kujionea

changamoto zinazoikabili.

 

DC alisema  hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwamo upungufu wa vifaa tiba na  dawa.

 

Alisema watumishi wa hospitali hiyo pia hawawajibiki ipasavyo hivyo kusababisha wagonjwa kutopata huduma bora

za afya.

 

Mkuu huyo wa wilaya alisema   licha ya kukabiliwa changamoto hizo,  hawana budi kufanya kazi kwa bidii na kuonyesha upendo na upole kwa wagonjwa kwa kutoa huduma  bora.

 

Alisema huduma hiyo  iwe ni  pamoja na kuwaelimisha

watumiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii wanapofika kutibiwa   hospitalini hapo.

 

“Zipo changamoto zinazoikabili hospitali yetu ya Wilaya ya Maswa pia wapo wananchi wetu ambao ni wagonjwa waliojiunga na mifuko ya bima ya afya na mfuko wa afya ya jamii kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

 

“Lakini wanapofika katika hospitali yetu hawapatiwi elimu juu ya huduma wanazopaswa kuhudumiwa na wakati mwingine hujikuta wanalipia matibabu   mara mbili  jambo ambalo si zuri,” alisema.

 

Alimwagiza Kaimu  Mganga Mkuu wa wilaya hiyo,   Dk. Vedastus Luguga kuwachukulia hatua kali za  nidhamu na kuhakikisha anasimamia suala la kutolewa  huduma bora

za afya kwa wagonjwa.

 

Alisema  serikali wilayani humo imejipanga kukabiliana na

changamoto za upatikanaji wa  dawa na vifaa tiba kwa kuanzisha duka kubwa la  dawa   ndani ya hospitali hiyo.

 

“Hii ni hospitali kubwa na inatoa huduma hadi kwa baadhi ya wananchi wa wilaya jirani za Itilima na Meatu mkoani Simiyu na wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ambazo zinapakana na wilaya ya Maswa,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles