25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

DAKTARI ADAI ALIYETOBOLEWA MACHO NA ‘SCORPION’ ALITOBOLEWA UTUMBO

 

 

 

NA TUNU NASSOR

SHAHIDI katika kesi inayomkabili Salum Njwete maarufu ‘Scopion’, Daktari wa Kitengo cha Upasuaji cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk. Amin Abdulrahman ameiambia mahakama kuwa Saidi Mrisho alitobolewa utumbo mwembamba.

Akitoa ushahidi mbele ya hakimu Flora Haule Dk. Abdulrahmani alisema Septemba 7, mwaka jana saa 12 alfajiri akiwa chumba cha upasuaji alipigiwa simu na kitengo cha dharura cha hospitalini hapo kumtaka kwenda kumhudumia mgonjwa wa dharura.

“Baada ya kumfanyia uchunguzi niligundua anahitaji kufanyiwa upasuaji kutokana na jeraha kubwa lililokuwa kushoto mwa tumbo lake lililokuwa na urefu wa sentimita 30 kutoka katika ngozi ya ndani ya tumbo lililotoboa utumbo mwembamba na mengine madogo ambayo yalishonwa na kitengo cha dharura,” alisema Dk. Abdulrahman.

Alisema alifungua tumbo na kuliziba tundu hilo kasha kufunga tumbo na kumpeleka wodi namba 13 na kumpa rufaa kwa wataalamu wa macho kuendelea na uchunguzi wa majeraha ya machoni. Kesi hiyo itatajwa tena Machi 8, mwaka huu.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles