33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Coca cola yawazawadia wanafunzi kampeni Rejesha ushinde

FERDNANDA MBAMILA, DAR ES SALAAM

Kampuni ya Coca cola nchini kupitia mmoja wa washiriki wake Coca cola kwanza imekabidhi zawadi kwa wanafunzi katika Mkoa wa Dar es Salaam baada ya shule hizo kukusanya chupa za plastiki kupitia kampeni ya Copa Coca cola ya rejesha na ushinde.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Masoko  na Mauzo wa  Kampuni ya  Coca cola kwanza, Josephine Msaliwa aliwasihi  na kuwahamasisha wanafunzi na watanzania  kwa ujumla  kuendelea kushiriki kampeni za ukusanyaji wa chupa za plastiki na kampeni nyingine za namna  hiyo ili kupunguza taka  na kujenga mazingira safi na  yenye afya.

Alisema kwa shule zilizoshinda katika uokotaji wa  makopo ya plastiki zilikusanya zaidi ya chupa kilo 880,835 kwa Mkoa wa Dar es Salaam na Iringa ambapo shule ya sekondari Kihesa  ilipata idadi kubwa zaidi ya ukusanyaji wa chupa za plastiki na kushinda zawadi kubwa ambayo ni urekebishaji wa  kiwanja cha  mpira na zawadi nyingine mbalimbali.

Sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu  mashindano ya Coca cola yalikuwa zaidi ya mpira wa miguu kwa shule zote zilizoshiriki.

Aidha  mashindano  yalijikita zaidi  katika  kubadili tabia  kwa wanafunzi  kwa kuja  na kampeni  ya ukusanyaji kama sehenu ya  kuwaelimisha  juu ya umuhimu wa  usafi wa mazingira  kupitia ujusanyaji wa chupa.

Kwa Mkoa wa Dar es Salaam shule tatu zilifanya  vizuri  ikiwa ni pamoja na  shule ya  Sekondari ya Kisarawe  11 ya Wilaya  ya Kigamboni , Shule ya  Sekondari ya Kambangwa ya Kinondoni na   shule ya Sekondari ya  Mikwambe  ya Wilaya ya  Temeke.

“Wanafunzi wa shule hizo tajwa walikusanya kiasi cha chupa  za plastiki kilo 7,052, 6,279 na 3, 110 hiyo ni wakati wa kampeni  na ambapo siku ambapoyo walipewa zawadi ya jezi  32 za COPA Coca cola na mipira 2 kwa kila shule.

Pia wanafunzi watatu kutoka  kila moja ya  shule zilizoshinda, walipewa zawadi  za Tablet na saa kwa kuwa na ushawishi  mkubwa  katika shule zao, huku waalimu watatu  kutoka  kula shule  wakiondoka na zawadi za Laptop, beg na fulana za Coca cola.

Alisema ukusanyaji wa chupa  haulindi tu maliasili ya ulimwengu lakini pia husaidia  kuleta maisha  bora kwa kila mtu.

“Kama kampunu ya Coca cola tuliona  ni sawa  kuhamasisha wanafunzi  wanaoshiriki katika COPA Coca cola  kushiriki katika ukusanyaji  wa chupa za plastiki kutoka kwenye umri  mdogo ili kuleta  mabadiliko ya tabia  ndani yao katika maisha yao yote,” alisema Josephine.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles