27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

CHRIS BROWN KUSAIDIA WAJAWAZITO

NEW YORK, MAREKANI

MKALI wa muziki wa RnB nchini Marekani, Christopher Maurice ‘Chris Brown’, ametangaza kusaidia wanawake wajawazito kwenye huduma mbalimbai za afya nchini Marekani.

Msanii huyo aliweka wazi kuwa, katika maisha yake ndoto kubwa ni kusaidia huduma za afya kwa wanawake hasa wale wenye ujauzito.

“Furaha yangu ni kuona nasaidia wanawake kwenye huduma za afya, wengi wao wamekuwa katika wakati mgumu hasa wakiwa wajawazito kwa kuwa wanatakiwa kuhudhuria mara kwa mara kwenye huduma za afya.

“Tangu nikiwa mdogo nimekuwa na wazo hilo la kuja kusaidia, nashukuru ndoto zangu zimetimia na ninatarajia kufanya hivyo hivi karibuni kwenye sehemu mbalimbali za huduma za afya,” alisema Brown.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles