23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

CDF Mabeyo ateua timu ya kusomba korosho

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Jenerali Venance Mabeyo, amemteua Meja Jenerali, George Msongole, kusimamia zoezi zima la kuhamisha korosho.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 17, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Yacoub Mohamed, amesema Meja Jenerali Msongole atakuwa na timu yake.

“Mkuu wa Majeshi alitengeneza utaratibu wa kazi itakavyofanyika na alimteua Meja Jenerali, Msongole ambaye atakuwa na timu yake ambayo tayari iko hapa,” amesema Luteni Jenerali, Mohamed.

Tayari magari kadhaa ya JWTZ yatakayosomba korosho hizo yamewasili mkoani Mtwara.

Magari hayo yatasomba korosha kutoka kwenye maghala makuu na kuzipeleka katika maeneo maalumu yaliyoandaliwa kusubiri shughuli ya ubanguaji.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles