23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Cardi B amjaribu Minaj kwa Meek Mill

MIAMI, MAREKANI

Staa wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Belcalis Almánzar ‘Cardi B’, amepanga kuachia wimbo mpya aliomshirikisha mpenzi wa zamani wa Nicki Minaj, Meek Mill.

Cardi B na Nicki Minaj wamekuwa kwenye mgogoro kwa miezi kadhaa sasa, lakini Cardi B anaonekana kutaka kuendeleza bifu lao baada ya kutangaza kuwa anataka kuachia wimbo na aliyekuwa mpenzi wa msanii huyo.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Cardi B na Meek Mill wamekamilisha wimbo wao ambao unajulikana kwa jina la ‘Hooks and Verses’, hivyo mashabiki wa msanii huyo wanausubiri kwa hamu kubwa.

Hata hivyo, hajaweka wazi kuwa kazi hiyo ataiachia lini lakini mashabiki wanaamini wimbo huo utazidi kuchochea bifu la warembo hao ambao wanafanya muziki wa hip hop.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles