24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Cannon ampongeza Mariah kuvishwa pete

Hennessy V.S Hosts A Special Dinner With Nick CannonNEW YORK, MAREKANI

MPENZI wa zamani wa Mariah Carey, Nick Cannon, amempongeza mke wake huyo wa zamani kwa kuvishwa pete ya uchumba na bilionea, James Packer.

Cannon mwenye umri wa miaka 35, juzi aliweka picha ya Mariah Carey katika akaunti yake ya Instagram akimpongeza kwa kitendo hicho cha uchumba wake mpya.

“Hongera sana Mariah Carey kwa kuvishwa pete na James, nawatakia maisha mema yajayo na katika muungano wenu,” aliandika Cannon.

Cannon na Mariah walifanikiwa kupata watoto wawili wakati wa uhusiano wao ambao ni mapacha wenye umri wa miaka minne, Moroccan na Monroe.

Mume huyo wa Mariah, James, anakadiriwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 4.5, huku uhusiano wao unadaiwa kuanza muda mrefu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles