31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

CANNAVARO KUMRITHI LWANDAMINA YANGA

Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM

NAHODHA wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amefichua kuwa anakusudia kusomea ukocha baada ya kustaafu soka.

Akizungumza na MTANZANIA, Cannavaro alisema anataka kusomea taaluma hiyo ili aje kuchukua mikoba ya kocha wake wa sasa wa timu hiyo, George Lwandamina.

Cannavaro ambaye tangu kuanza kwa msimu huu wa Ligi Kuu hajaichezea Yanga mchezo hata mmoja, amekuwa akijifunza vitu vingi kutoka kwa kocha wake huyo ambavyo anaamini vitamsaidia pale atakapoamua kufanya kazi ya kufundisha.

“Hakuna kinachoshindikana kwani katika kipindi cha misimu 11 nilichoichezea  Yanga nimejifunza mambo mengi.

“Kwa kuwa lengo langu ni kusomea ukocha baada ya kustaafu naamini yatanisaidia sana katika kuifanya kazi kwa ufanisi,” alisema.

Cannavaro alijiunga na Yanga mwaka 1997 akitokea timu ya Tembo ya Zanzibar.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles