25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Canelo sasa amsubiri  Gennady

saul-canelo-alvarezTEXAS, MAREKANI

BONDIA  wa uzito wa kati, Saul ‘Canelo’ Alvarez, jana  amefanikiwa  kumdunda mpinzani wake, Liam  Smith, katika  mzunguko wa tisa  wa pambano la uzito wa kati la kugombea  mkanda wa  WBO  lililofanyika jijini Texas, Marekani.

Kipigo hicho  kilichokuwa kikishuhudiwa na zaidi ya watu  51,240, kilikuwa cha mara ya kwanza kwa Smith  ambaye aliwahi  kushinda mapambano  nane  kwa ‘knock out’.

Baada ya ushindi huo, sasa  Canelo anatarajia kupambana na  bondia machachari, Gennady Golovkin,  ambaye  amekuwa akisubiri  kwa muda mrefu kuzichapa na nyota huyo.

Alvarez ambaye kwa sasa anaonekana kuwa  katika kiwango bora cha ngumi, kabla ya pambano  hilo alitarajiwa kupambana na  Oscar De La Hoya na  Golden Boy.

“Kama  nitaendelea kusubiri kwa muda mrefu  na kupata uzoefu wa kutosha, nitaweza kupambana kwa kiwango bora kama nilichokionesha  katika mchezo huu, hata hivyo  nilichukizwa sana na matokeo haya ingawa  Canelo alikuwa bora zaidi yangu na alinishinda kimbinu,” alithibitisha  Smith baada ya kudundwa na Canelo.

“Ilinichukua muda mrefu kujibu mapigo, lakini niligundua sikuwa na mbinu za kutosha na kumfanya adui yangu afikiri mara mbili  kwani  mwenzangu aliweza kumudu kila kitu,” alisema Smith.

Kwa upande wake, Canelo alisema ndoto yake ya kushinda  pambano hilo  ilifanikiwa kwa kujituma kwa bidii akiwa ulingoni.

“Niliahidi kwamba ningeshinda pambano hili na kuwa bingwa kama ilivyotokea leo, nilipambana ingawa nilikuwa katika mazingira magumu ulingoni.

“Niliumia mkono wangu wa kulia, hivyo ilinilazimu kutumia wa kushoto  mara kwa mara,” alisema Canelo na kuongeza kuwa mpinzani wake alikuwa makini ulingoni, alikuwa akifikiri kabla ya kurusha ngumi dhidi yake.

Canelo alisema kuna wakati alilazimika kutumia mkono wa kushoto ili kutunza nguvu mkono wa kulia.

“Niliumia mkono wa kulia katika mzunguko wa pili wakati niliporusha ngumi iliyotua juu ya kichwa cha mpinzani wangu,” alisema Canelo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles