30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

BUNGE LAWAAGIZA HECHE, ZITTO KURIPOTI POLISI

Gabriel Mushi, Dodoma

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amemtaka Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema) na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT- Wazalendo) kwenda kuripoti polisi taarifa zao za kutishiwa uhai.

Pia amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kufuatilia kwa karibu taarifa hizo za wabunge kutishiwa uhai.

Agizo hilo la Naibu Spika limetolewa leo bungeni mjini Dodoma wakati akitolea ufafanuzi mwongozo wa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) aliyeiomba serikali itoe maelezo kuhusu taarifa za wabunge hao kutishiwa uhai.

Waitara amesema licha ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kusema wabunge wako salama, taarifa zilizopo kwenye vyombo vya habari ni kwamba wabunge hao wamesema wanafuatiliwa na watu wanaowatishia uhai hivyo wakapewa nafasi ndani ya bungeni kuelezea taarifa hizo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles