24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

BoT yahamishia mali, madeni ya Bank M kwenda Benki ya Azania

Anna Potinus, Dar es Salaam

Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeifungia kutoa huduma Bank M kutokana na kushindwa kufuata masharti waliyowekewa ikiwamo la ukwasi na hivyo mali na madeni ya benki hiyo yamehamishiwa kwa Benki ya Azania Bank.

Kaimu Gavana wa BoT, Dk. Bernad Kibese, amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“BoT inapenda kuutangazia umma kwamba imeamua kuwa mali na madeni ya Benki M yatachukukiwa na mtu mwingine ambaye ni Azania Bank Limited, kama ufumbuzi wa matatizo ya benki hiyo,” amesema Dk.Kibese

Aidha, amesema BoT haitasita kuingilia kati pale itakapoona benki yoyote inaelekea pabaya, pia amewataka wateja wote wenye madeni kuendelea kuyalipa kulingana na mikataba yao.

“Wateja wenye amana watatangaziwa tarehe ya kuanza kupata huduma za kibenki kupitia Benki ya Azania, na wale wenye mikopo wanatakiwa kuendelea kulipa mikopo hiyo kwa mujibu wa mikataba yao na Benki Kuu italisimamia hilo,” amesema Dk. Kibese.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles