31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Batuli: Wazazi wanafurahia nguo za utupu

Na Festo Polea
MWIGIZAJI Yobnesh Yusuf maarufu kwa jina la Batuli, ameweka wazi kwamba tabia ya waigizaji wa kike kuvaa nguo za nusu uchi huwa zikifurahiwa na wazazi wa waigizaji hao.
Batuli alieleza hayo baada ya kuulizwa kwanini waigizaji wa kike wanapendelea mavazi ya nusu uchi wachezapo katika filamu zao.
“Hapo tatizo ni wazazi wa waigizaji hao wanaovaa nguo hizo wanaonyesha wanafurahia, kama wangechukizwa na tabia hiyo wasingevaa nusu uchi na kuiahibisha tasnia nzima na wanawake kwa ujumla,” alieleza Batuli.
Batuli mwenye ndoto ya kuasili mtoto wa kike, aliongeza kwa kuwataka waigizaji wenzake wavae mavazi ya kujitambua na yenye stara kwao, wazazi wao na jamii inayowazunguka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles