30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

ARIANA GRANDE KUSAIDIA MAZISHI YA WATU 22

 

 

LONDON, ENGLAND 

STAA wa muziki nchini Marekani, Ariana Grande, ameeleza kwamba yupo tayari kusaidia mazishi ya watu 22 waliopoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu, mara baada ya kumalizika kwa onyesho lake la muziki nchini Uingereza.

Watu 22 walipoteza maisha na wengine 119 walijeruhiwa kwa tukio la kigaidi la mlipuko wa bomu lililotokea kwenye Ukumbi wa Manchester Arena nchini Uingereza, ambapo msanii huyo alikuwa akifanya onyesho hilo ikiwa ni ziara yake ya muziki aliyoiita ‘The Dangerous Woman Tour’.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, msanii huyo amedai kuungana na familia za watu hao waliopoteza maisha ili atoe mchango wake wa kifedha katika mazishi yao.

“Nimefanya mazungumzo na familia za marehemu na nimewaomba nichangie katika shughuli za mazishi kwa kuwa marehemu wamepatwa na umauti baada ya kuhudhuria onyesho langu, nitaungana nao katika kipindi hiki kigumu kwao,” aliandika Ariana. 
 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles