24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Alonso apongeza falsafa ya Guardiola

downloadMunich,Ujeruman

KIUNGO wa Bayern Munich Xabi Alonso ameipongeza falsafa ya soka ya kocha anayetarajiwa kuondoka Bayern Pep Guardiola  kwa kuamini  kuwa msingi thabiti alioutengeneza  katikma timu hiyo  utadumu kwa muda mrefu hata baada ya kuondoka kwake.

Kocha huyo wa Kihispania ameanza kampeni nyingine ya kuwa mtawala katika soka huku mataji matatu yakiwa ndani ya uwezo wake msimu huu, lakini atatimkia Uingereza kuchukua kibarua cha Manchester City majira ya joto.

Baadhi ya mashabiki wa Bayern waliukosoa mfumo wa kocha huyo ambao umeegemea katika kumiliki mpira lakini Alonso amesema kikosi kizima sasa kinakubaliana na maono ya Guardiola.

“Inaweza isiwe rahisi kukwambia, kwa sababu Pep yupo mbele ya wakati. Kocha huyo anahitaji mafanikio yake binafsi na ya wachezaji pia,,”  alisema Alonso.

“Lakini mara utakapoelewa, kama kwa upande wangu hivyo ndivyo tunavyopenda kucheza. Tunapenda kucheza kwa kumiliki zaidi, naye anapenda hivyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles