26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Murray achukua ubingwa wa Davis Cup

76_muz_1539494aLONDON, ENGLAND

NYOTA wa mchezo wa tenisi nchini Uingereza, Andy Murray, amefanikiwa kulipa taifa lake ubingwa wa michuano ya Davis Cup katika mchezaji mmoja mmoja.

Timu ya Uingereza imetwaa taji hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1936, huku Murray akifanikiwa kumshinda mpinzani wake raia wa Ubelgiji, David Goffin.

Murray alimshinda mapinzani huyo kwa jumla ya seti 6-3, 7-5, 6-3 na kumfanya Goffin kupoteza kwa jumla ya seti 3-1.

Murray amejiongezea historia kubwa baada ya kutwaa mataji ya michuano ya Wimbledon, michuano ya wazi ya US Open na ile ya Olimpiki.

Mchezaji huyo amekuwa na furaha kubwa ya kulipa taifa lake ubingwa huo, huku akidai kuwa hawezi kuamini kilichotokea.

“Nina hisia kali sana na siwezi kuelezea, ninaamini itachukua muda mrefu kuweza kupungua kwa hisia hizo, maana nina furaha kubwa ambayo itaendelea maishani mwangu.

“Haikuwa kazi rahisi kuweza kushinda kwa kuwa mchezo ulikuwa mgumu, lakini kwa upande wangu ninashukuru nimefanikiwa kutwaa taji hilo na kuliwakilisha vema taifa langu,” alisema Murray.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles