25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Kardashian ahofia kupata kisukari

kim-kardashianNEW YORK, MAREKANI

MKE wa Kanye West, Kim Kardashian, amehofia kupata ugonjwa wa kisukari kutokana na ulaji wake wa ovyo wa vyakula vya aina mbalimbali kipindi hiki cha ujauzito wake.

Mrembo huyo anatarajia kupata mtoto wa pili kabla ya Desemba 26.

“Ninaamini nina afya njema, lakini kuna wakati najikuta nakula bila mpangilio hivyo naweza kupata ugonjwa wa sukari, ninaamini hali hii inatokana na ujauzito na ndiyo maana muda mwingi natamani kula,” alisema Kim.

Hata hivyo, mrembo huyo atakuwa na furaha kubwa ya kuongeza familia yake hivi karibuni. “Familia inatarajia kuwa kubwa muda mfupi ujao, kwa sasa tupo watatu, lakini hadi kufika Desemba 27 tutakuwa na familia ya watu wanne,” aliongeza Kim.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles