30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

‘Yatima Hadeki’ kuingia mtaani Desemba

Festo KiseNA CHRISTOPHER MSEKENA

MSANII chipukizi wa filamu nchini, Festo Kise ‘Kise’, anatarajia kuingiza sokoni filamu yake ya kwanza inayoitwa ‘Yatima Hadeki’ inayohusu mateso, misukosuko na mafunzo mbalimbali kwenye maisha ya Mtanzania.

Kise alisema hiyo ndiyo filamu yake ya kwanza kuiandaa na kucheza kama mhusika mkuu huku akitarajia kwamba italeta changamoto kwa wasanii wakubwa kutokana na maudhui ya hadithi yenyewe.

“Hii ni filamu yangu ya kwanza, naamini mashabiki wa filamu wataipokea vyema kwa sababu hadidhi yake ina mafunzo mbalimbali kwa jamii, itaongeza hamasa ya kufuatilia filamu za Tanzania kutokana na mafunzo yake,” alieleza.

Katika filamu hiyo pia wapo wasanii wenye majina makubwa nchini akiwemo Mzee Msisili, Swahib Suleiman na Barafu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles