25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Lil Wayne: Birdiman anawatesa wasanii

Lil-Wayne na BirdmanNEY YORK, MAREKANI

NYOTA wa muziki nchini Marekani, Dwayne Carter ‘Lil Wayne’, amemshambulia bosi wa kundi la Cash Money, Bryan Williams ‘Birdman’ ambaye ni kama baba yake mlezi.

Lil Wayne alilelewa na Birdman kuanzia alipokuwa na umri mdogo hadi alipopata mafanikio akiwa chini ya kundi la Cash Money na kisha kuanzisha kundi lake la Young Money.

Lakini wawili hao kwa sasa hawana uhusiano mzuri na kila mmoja anafanya kazi peke yake, kutokana na hali hiyo, Lil Wayne amefunguka na kusema kuwa Birdman anawanyonya wasanii wenzake ambao ni Nick Minaj, Drake, Tyga na wengine.

“Birdman anawatesa wasanii kwa kuwa wanafanya kazi kubwa lakini malipo yao ni madogo, namjua kwa kuwa nimekaa naye kwa miaka mingi, hivyo wasanii wa kundi hilo wanatakiwa kuwa makini na kazi zao,” alisema Lil Wayne.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles