31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Samatta anukia ufungaji bora Afrika

samataNA ABDUCADO EMMANUEL, DAR ES SALAAM

MTANZANIA Mbwana Samatta, anayekipiga katika timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, amebakisha mabao mawili tu kuweza kutwaa kiatu cha ufungaji bora wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka huu.

Mpaka sasa timu yake ikiwa imeingia fainali ya michuano hiyo, Samatta anashika nafasi ya pili kwenye chati ya ufungaji bora akiwa na mabao sita, sawa na Mouhcine Iajour wa timu ya Moghreb Tetouan ya Morocco iliyotolewa, anazidiwa bao moja tu na kinara Bakri Al-Madina anayekipiga El Merreikh ya Sudan aliyetupia saba.

TP Mazembe inatarajia kucheza na USM Alger ya Algeria katika fainali ya michuano hiyo, mchezo wa kwanza utafanyika kati ya Oktoba 30 na Novemba mosi, mwaka huu huku wa marudiano ukifanyika kati ya Novemba 6 na 8 mwaka huu.

Mshambuliaji huyo, 23, ana nafasi ya kumzidi Al Madina kama atafanikiwa kufunga mabao mawili katika mechi mbili zijazo za fainali watakazocheza dhidi ya USM Algier.

Wachezaji wanaoweza kuyafikia mabao ya Samatta ni mshambuliaji mwenzake wa TP Mazembe, Roger Assale, aliyefunga matano, Youcef Belaili (USM Algier) aliyetupia manne sambamba na Kaddour Beldjilali na Mohamed Meftah (USM Alger) waliotupia matatu kila mmoja.

Mwaka jana mshambuliaji mwingine wa Tanzania, Mrisho Ngassa, aliyekuwa akikipiga Yanga alikuwa ni miongoni mwa wafungaji bora wa michuano hiyo kwa mabao yake sita, akilingana na wenzake watatu, El Hedi Belameiri (ES Setif, Algeria), Haythem Jouini (Esperance, Tunisia) na Ndombe Mubele (AS Vita, Kongo).

Samatta anayecheza TP Mazembe sambamba na Mtanzania mwingine, Thomas Ulimwengu, wana nafasi ya kuandika rekodi ya kuwa Watanzania wa kwanza kutwaa ubingwa huo mkubwa wa Afrika kwa ngazi ya klabu kama wataifunga USM Algier.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles