29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Msanii wa Kenya afariki visiwa vya Mbudya Dar

ShrekeezyNAIROBI, Kenya

MSANII wa muziki wa genge nchini Kenya, Simon Njoroge ‘Shreekezy’, amepoteza maisha akiwa jijini Dar es Salaam katika visiwa vya Mbudya vilivyopo Bahari ya Hindi.

Msanii huyo anadaiwa kufariki Agosti 30 baada ya boti aliyokuwa akiiendesha baharini akitokea Hoteli ya Whitesands kuelekea visiwa hivyo kumtupa ambapo alifariki dunia na mwili wake ulipatikana baada ya siku tatu.

Msanii huyo alikuwa nchini Tanzania kwa siku nane kabla ya kifo chake kutokea. Hata hivyo, inadaiwa katika boti hiyo alikuwa na mwanamke wa kizungu ambaye alishindwa kumuokoa wakati wa ajali hiyo ilipowatokea.

Msanii huyo mwaka 2011 aliwania tuzo ya msanii mwenye kipaji nchini Kenya katika tuzo za Chaguo la Teeniez.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles