27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Msajili awaonya wanasiasa wanaokiuka makubaliano

mutungiNa Mauli Muyenjwa, Dar es Salaam

MSAJILI wa Vyama vya Siasa,  Francis Mutungi amesema  licha ya  uchaguzi wa mwaka huu kughubikwa na ushindani, muda muafaka ukifika rungu litawadondokea wanasiasa wanaokwenda kinyume na makubaliano waliyoyasaini.

Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam  jana wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa mawakala wa usimamizi wa vyama vya siasa ya kuwaandaa katika uchaguzi mwaka wa mwaka huu.

“ Tuelewe kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi, wanasiasa wafanye amani iwe kipaumbele na kila mtu ana wajibu   kuufanya uchaguzi kuwa salama… chama kinapokosea kitaadhibiwa,” alisema Mutungi.

Alisema   mawakala wapatao 1,300 kutoka katika vyama vya siasa watapatiwa mafunzo hayo katika siku zijazo na    30 walianza  mafunzo hayo jana.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) ambalo ni wadhamini wa mafunzo hayo, Awa Dabo, alivishukuru vyama vya siasa akisema  mawakala hao wakifundishwa  watajiamini na matokeo ya uchaguzi yatakua ya kweli na ya haki.

“Mawakala kutoka katika vyama vya siasa wanatakiwa kujua sheria za uchaguzi na utaratibu.  Wanahitaji kufundishwa  waweze kushiriki vizuri katika mchakato huo lakini pia wanatakiwa kujua haki zao na wajibu katika utendaji na mamlaka yao,” alisema Dabo.

 

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, Peter Mziray alisema     ikitokea kuvunjika   amani na purukushani nchini,  baraza la vyama vya siasa lazima lilaumiwe kwa vile  linahusisha vyama vyote.

Akizungumza kwenye ufunguzi huo,  Mwenyekiti  wa Chama cha UMD, Kamana Masoud, alisema  uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu kuliko wa miaka yote iliyopita na   kuna wasiwasi mawakala kuweza kununuliwa na kuchakachua kura.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles