25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Mwanafunzi darasa la nne ajinyonga chumbani

Na Asifiwe George, Dar es Salaam

MWANAFUNZI wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Pugu jijini Dar es Salaam, Festo Filbert (11) amekutwa chumbani kwake akiwa amejinyonga hadi kufa kwa kutumia mkanda wa kuvalia nguo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Mary Nzuki alisema tukio hilo lilitokea jana katika eneo la Majohe kwa Ngozoma.
Alisema sababu za kujinyonga mwanafunzi huyo bado hazijafahamika kwani hakuacha ujumbe wowote.
“Mtoto huyu alikutwa chumbani kwake anakolala akiwa peke yake, hakuna aliyejua sababu za kifo chake,” alisema.
Alisema maiti ya mwanafunzi huyo, imehifadhiwa Hospitali ya Amana na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles