24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mengi atuhumiwa kwa uhaini *Mwenyewe aibuka na kukanusha

Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam
MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, ametuhumiwa kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu.

Baada ya tuhuma hizo kuelekezwa kwake na gazeti la Taifa Imara lililochapishwa Machi 23, mwaka huu likiwa na kichwa cha habari kinachosema, ‘Zitto amchongea Mengi kwa JK? Mwenyewe ameibuka Dar es Salaam jana na kuzikanusha mbele ya waandishi wa habari akisema zimemshtua na kumuogopesha.

“Tuhuma zilizotolewa na gazeti la Taifa Imara la Machi 23-29, mwaka huu kwamba nina nia ya kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi, zimenishtua sana,” alisema Mengi.

Alisema habari hiyo imempa hofu kubwa juu ya mustakabali wa maisha yake kutokana na kile kilichoandikwa kuwa Kikwete aliapa atapambana naye.

“Hofu yangu kubwa inasababishwa na Ikulu na Maelezo kwa kukaa kimya kwa zaidi ya wiki tatu bila kutoa ufafanuzi.

“Ikulu na Maelezo wako makini katika kutoa ufafanuzi wa haraka wa jambo lolote linalomhusu Rais Kikwete, lakini katika hili nashangaa kuona taasisi hizo zimeamua kukaa kimya na kuacha tuhuma hizo kusambaa,” alisema Mengi.

Alisema hofu yake inazidi kuwa kubwa zaidi kwa sababu Kikwete ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, hivyo kauli yake kama ilivyonukuliwa na gazeti hilo atapambana naye inaweza kuchukuliwa kama agizo kwa vyombo vya dola na kumuangamiza.

Pamoja na mambo mengine, habari hiyo ilisema Zitto Kabwe amemchongea Mengi kwa Kikwete kuwa ndiye kinara wa kuhujumu Serikali yake.

Habari hiyo iliyoeleza kuwa chanzo chake ni Ikulu, iliendelea kudai kuwa Zitto alikutana na Kikwete muda mfupi baada ya kuwasilisha bungeni Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow wakati huo akiwa ni mwenyekiti.

Habari hiyo ilidai katika mazungumzo yake na Kikwete, Zitto alinukuliwa akimueleza kuwa anayesababisha Serikali yake iyumbe mara kwa mara ni Mengi.

“Zitto amekuwa akishawishiwa na Mengi kuiangusha Serikali ya Kikwete na alikwenda mbali zaidi kumwambia rais kwamba, Mengi ameapa kuwa kiongozi huyo akimaliza muda wake wa urais atamshughulikia kwa nguvu zake zote,” ilisema sehemu ya habari hiyo.
Habari hiyo ilisema baada ya maelezo hayo, Kikwete aliapa kupambana na Mengi na akamshukuru Zitto kwa kumpa taarifa hizo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles