31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

SERENGETI YAHITAJI ZAIDI YA TANI 4 ZA CHAKULA

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu
Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu

Na MALIMA LUBASHA – SERENGETI

ZAIDI ya tani 4.1 za chakula zinahitajika wilayani ya Serengeti mkoani Mara ili kunusuru maisha ya kaya zaidi ya 32,000 kutokana na mahindi yao  kukauka kutokana na ukame.

Akizungumza  na waandishi wa habari ofisini kwake  juzi, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu alisema hali ya chakula  kwa mwaka huu sio ya kuridhisha kutokana na  mvua vuli  kutonyesha kwa wakati.

Alisema wapo  baadhi ya watu, wanakula mlo mmoja na wengine mitatu kwa siku na hakuna mtu wala mifugo iliyokufa kutokana na ukame, kwa sasa bei ya mahindi debe moja linauzwa  Sh 15,000 ambapo upatikanaji wa chakula kwenye masoko wa kiwango kinachohitajika.

Alisema wilaya bado inaendelea kufanya tathimini kwa kupita kila kaya ili kubaini hali ya chakula kwa wale wenye upungufu wa chakula, kaya zisizo na uwezo,zenye uwezo na zile zinazohitaji msaada wa chakula  na tayari wameomba kibali ili wafanyabiashara waruhusiwe kuuza mahindi kwa bei nafuu.

“Maofisa kilimo wamefanya tathimini kwenye  kaya 32,055 zilizopo katika  kata 22 kati ya 30,wamebaini kaya 8,582 ambazo ni maskini  zinahitaji chakula cha bure tani 811, kaya 10,655 wenye hali ya nafuu wanahitaji tani 1,454.4 na kaya 12,818 zilizo na uwezo wa kununua kwa bei yoyote zinahitaji tani 1,749.7 za mahindi,” alisema Babu.

Hata hivyo, Babu  amewataka wananchi kuhifadhi chakula kilichopatikana na kuacha utamaduni wa kutumia nafaka kutengenezea pombe za kienyeji na kila familia iwe na ghala la kuhifadhi chakula.

Alisema mbali ukame, mvua kutonyesha kutokana na mabadiliko ya tabianchi pia yapo malalamiko ya wananchi kuhusu tembo kuvamia mashamba yao na kula mazao yote na kueleza kuwa changamoto hiyo serikali inalifahamu na takwimu za uharibifu zilikwisha wasilishwa wizara ya maliasili na utalii ili kuli pa kifuta machozi kwa wote walioathirika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles