YERUSALEM, ISRAEL
WAZIRI Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, anakabiliwa na shinikizo zaidi kufuatia madai ya ufisadi baada ya gazeti moja ya Israel kuripoti kuwa polisi wana kanda ya sauti ya Netanyahu ambayo inayaunga mkono madai hayo.
Awali Netanyahu alisema kuwa madai hayo hayana msingi wowote.
Gazeti la Haaretz, hata hivyo limechapisha madai kuwa sasa polisi wana kanda ya sauti ambapo Netanyahu anaripotiwa kusikika akiongea kwa njia ya simu na mfanyabiashara mmoja.
Hata hivyo madai hayo hayajathibitishwa rasmi.