33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Barcelona, Man City hapatoshi leo

barcelona-man-cityBARCELONA, HISPANIA

USIKU wa Ulaya unatarajia kuendelea leo kwa michezo nane kupigwa katika viwanja mbalimbali, huku mchezo unaotarajiwa kugusa hisia za watu wengi ni kati ya Barcelona ambao watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani dhidi ya Manchester City.

Mbali na kuwepo kwa michezo mingi leo, dunia itasimama kwa muda kwa ajili ya kuutazama mchezo huu ambao ni wa kiufundi.

Makocha wa timu hizo wote waliwahi kuitumikia klabu ya Barcelona wakiwa kama wachezaji, lakini leo hii wanakutana na kuonesha ufundi wao, Pep Guardiola akiwa kocha wa Manchester City, huku Luis Enrique akiiongoza Barcelona.

Guardiola alikuwa na mchango mkubwa akiwa na klabu ya Barcelona tangu mwaka 2008 hadi 2012 alipojiunga na Bayern Munich ya nchini Ujerumani, aliipa mafanikio makubwa ambayo yatakumbukwa kwa kiasi kikubwa.

Katika mchezo uliopita wa klabu bingwa, Man City walikutana na Celtic na kutoka sare ya 3-3, leo hii wanakutana na Barcelona ambayo mchezo wao uliopita waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Monchengladbach.

Hata hivyo, Pep Guardiola ameshindwa kuzuia hisia zake kwa klabu ya Barcelona ambapo ameweka wazi kuwa mchezo huo utakuwa mgumu sana kutokana na ubora wa wapinzani wake.

“Najua uwezo wa klabu ya Barcelona, ninaamini mchezo utakuwa mgumu sana ubora wa wenzetu upo juu tofauti na sisi, lakini chochote kinaweza kutokea kwenye soka.

“Naweza kusema kuwa Barcelona ni kama mashine, kuna wachezaji watatu ambao ni hatari katika safu ya ushambuliaji,” alisema Guardiola.

Kwa upande wa Enrique, alisema hajazungumza na Guardiola, lakini anaamini mchezo huu utakuwa wa aina yake kwa kuwa Guardiola ana uwezo mkubwa.

Michezo mingine ambayo itapigwa leo ni pamoja na Napoli itakayopambana na Besiktas, Arsenal itacheza na Ludogorets, wakati huo FC Rostov wakipambana na Atletico Madrid, Dynamo Kyiv dhidi ya Benfica, PSG watacheza na FC Basel, Monchengladbach watacheza dhidi ya Celtic na Bayern Munich watacheza na PSV Eindhoven.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles