24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Lowassa, Mbowe kuripoti polisi Jumanne ijayo

1

JOHANES RESPICHIUS-Dar es Salaam

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,   Simon Sirro, amesema viongozi wa juu wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliotakiwa kuripoti jana katika Kituo Kikuu Polisi  badala yake wataripoti Septemba 6, mwaka huu.

Viongozi hao ni pamoja na Mwemyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Mjumbe wa Kamati Kuu, Edward Lowassa, Katibu mkuu, Vincent Mashinji, Naibu wake, John Mnyika na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Said Issa Mohammed.

Akizungunmza na MTANZANIA kwa simu,  Sirro, alisema jeshi hilo linajua kuwa viongozi hao wa Chadema wanatakiwa kuripoti kituoni hapo Jumanne ijayo.

“Tumewaambia waripoti hapa kituoni siku ya Jumanne wiki ijayo… kuhusu kwa nini haikuwa leo waulize wao waliotakiwa kuripoti,” alisema.

Viongozi hao wa Chadema walikamatwa na polisi hivi karibuni wakiwa katika kikao maalum cha Kamati Kuu katika Hoteli ya Giraffe   Dar es Salaam. Walihojiwa na kutakiwa kuripoti jana katika kituo hicho.

Hata hivyo     gazeti moja linalotolewa kwa njia ya mtandao (jina tunalo) lilimkariri Kamanda Sirro akisema  kuwa baada ya Chadema kutangaza kusimamisha maandamano yao maarufu kama Ukuta, Jeshi la Polisi liliwataka waliokamatwa juzi kutokwenda kuripoti polisi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles