27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Henry: Ubelgiji kutanifanya niwe kocha bora

 Thierry Henry
Thierry Henry

LONDON, ENGLAND

BAADA ya Thierry Henry kuchaguliwa kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Ubelgiji, kocha huyo amedai kuwa nafasi hiyo itamfanya aje kuwa bora zaidi.

Timu hiyo kwa sasa ipo chini ya kocha wa zamani wa klabu ya Everton, Roberto Martinez, ambapo kocha huyo ameamua kumpa nafasi nyota wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry.

Awali, Henry alikuwa anaifundisha timu ya vijana ya Arsenal chini ya miaka 18, lakini aliachana nayo baada ya kupishana kauli na kocha mkuu wa klabu hiyo, Arsene Wenger.

Henry amedai kuwa alikuwa hawezi kukataa ombi la Martinez kumtaka kuwa msaidizi wake na anaamini nafasi hiyo itamfanya awe bora katika ukocha kwa kipindi kifupi kijacho.

“Naanza kwa kukishukuru chama cha soka nchini Ubelgiji na kocha Martinez kwa kunipa nafasi hii, ninaamini hii ni changamoto kwangu katika kazi ya ukocha.

“Kitu ambacho tunatakiwa kukifanya ni kuhakikisha ubora wa timu ya Ubelgiji unabaki pale pale na kuhakikisha inakuwa timu bora zaidi duniani.

“Nilikuwa namjua vizuri Martinez tangu siku za nyuma, hivyo ilikuwa ngumu kwangu kukataa ombi lake. Ninaamini nitaweza kufanya kile ambacho anakitaka na kumsaidia kuipeleka mbali timu hiyo.

“Ninaamini timu hiyo itakuwa na historia mpya kutokana na uwezo wa kocha mkuu na uongozi wake,” alisema Henry.

Mbali na kuwa kocha msaidizi wa timu hiyo, pia ni mchambuzi wa masuala ya michezo katika kampuni ya Sky Sport nchini England.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles