25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ciara: Future kanitibulia dili

Ciara Princess
Ciara Princess

CALIFORNIA, MAREKANI

NYOTA wa muziki nchini Marekani, Ciara Princess, ameweka wazi kuwa amepoteza zaidi ya dola 500,000 kutokana na mgogoro wake dhidi ya baba wa mtoto wake Future.

Wawili hao waliachana mapema mwaka huu na sasa Ciara amefanikiwa kufunga ndoa na mume wake Russell Wilson mwezi uliopita.

Mrembo huyo amesema baada ya kuachana na baba wa mtoto wake Future, walianza kushambuliana kupitia mitandao ya kijamii, hali hiyo ilimfanya apoteze kiasi hicho cha fedha kutokana na baadhi ya mikataba kuvunjwa.

“Maneno ambayo tulikuwa tunarushiana na Future yameleta madhara makubwa kwangu kwa kuwa kuna baadhi ya mikataba nilitakiwa kusaini lakini maneno ya Future yalikuwa makali na kuwafanya wawekezaji wangu wasitishe.

“Lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa na ninaamini nitaendelea kuwa sawa na watu wangu na kujipatia mikataba mipya,” alisema Ciara

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles