24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Nyumba ya Michael Jackson yawekwa sokoni

michael-jacksonLAS VEGAS, MAREKANI

NYUMBA iliyokuwa ya msanii wa Pop, Michael Jackson, imetangazwa kuuzwa kwa kitita cha dola milioni 9.5

Kabla Michael Jackson hajapoteza maisha, nyumba hiyo yenye eneo la mraba 24,276, aliipangisha tangu mwaka 2007 hadi anapoteza maisha mwaka 2009, lakini familia ya msanii huyo imetangaza kuiuza nyumba hiyo yenye vyumba 12.

Kristen Routh ambaye alikuwa ni meneja wa msanii huyo ameweka wazi kuuzwa kwa nyumba hiyo, huku fedha zikitakiwa kuwasaidia watoto wa marehemu.

Jackson aliacha watoto watatu wa kiume wakiwa wawili na wa kike mmoja ambao ni Prince Michael Jackson II, Paris-Michael Katherine Jackson na Michael Joseph Jackson Jr.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles