31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Amber Talk Show kumwalika Wiz Khalifa

Amber RoseNEW YORK, MAREKANI,

MWANAMITINDO maarufu nchini Marekani, Amber Rose, anatarajia kumwalika baba mtoto wake katika kipindi chake cha Amber Talk Show.

Mrembo huyo amedai kwamba atakuwa na furaha kubwa kumkaribisha mume wake wa zamani katika kipindi hicho kwa ajili ya kuelezea maisha yake.

Hata hivyo, kupitia akaunti yake ya Instagram, Wiz Khalifa amedai kwamba hatakuwa na mengi ya kuongea kama watu wanavyodhani.

“Nitaenda kupita tu, sitokuwa na muda wa kupoteza, lakini nashukuru sana kwa kunipa nafasi hiyo kuwa mgeni rasmi,” aliandika Wiz Khalifa.

Wawili hao walifanikiwa kupata mtoto wa kiume na kumpa jina la Sebastian, lakini baada ya muda waliachana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles