25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Janet Jackson atarajia mtoto wa kwanza

janet-jacksonNEW YORK, MAREKANI

NYOTA wa muziki, Janet Jackson, anadaiwa kuwa na ujauzito wa mtoto wake wa kwanza kama atajifungua salama.

Mrembo huyo anatarajia kufikisha miaka 50 baada ya wiki mbili.

Aprili mwaka huu aliweka wazi kwamba hana mpango wa kufanya muziki kwa sasa kwa kuwa ana lengo la kutulia na mume wake kwa ajili ya kupanga familia, hivyo atachelewa kurudi katika muziki.

Mapumziko hayo yanadaiwa kuzaa matunda ambapo inaonesha wazi kwamba ana ujauzito hivyo anatarajia kupata mtoto wake wa kwanza.

Hata hivyo, msanii huyo ameweka wazi jambo hilo kupitia wimbo wake mpya ambao unajulikana kwa jina la ‘Dammn Baby’ tangu 2008 msanii huyo aliweka wazi kutaka mtoto hivyo ndoto zake zinaweza kuwa zimetimia.

 

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles